Mnamo Novemba, utawala wa Trump ulibatilisha Hali ya Kulindwa kwa Muda (TPS) ambayo ilitoa ulinzi dhidi ya kufukuzwa kwa Wahaiti 60,000 waliokuja Marekani baada ya tetemeko kubwa la ardhi kupiga nchi yao. Leo ni kumbukumbu ya miaka minane tangu kutokea kwa tetemeko la ardhi lililoharibu Haiti mnamo Januari 12, 2010.